Insha kuhusu wizi/uvamizi

Mambo ya kuzingatia:

  • Uvamizi ulitokea wakati upi?
  • Ulitokea wapi? k.m. shuleni, nyumbani, hotelini, safarini, benkini, nk.
  • Hali ya uvamizi k.m. silaha zilitumiwa/damu ilimwagwa/watu waliuawa/ nk.

 

Mfano:

  • Uvamizi nyumbani: Mtiririko wa mawazo
  • Ni wakati wa usiku mchanga.
  • Mnapiga soga huku mkiota moto na watu wa aila yako.
  • Mvua inaendelea kunyesha.
  • Ghafla mlango wa jikoni unagongwa kwa nguvu na kuvunjika.
  • Watu walio na silaha kali kali wajitoma jikoni.
  • Amri zinatolewa na wavamizi.
  • Risasi kufyatuliwa.
  •  Kamsa kupigwa na baadhi yenu.
  • Kujeruhiwa kwa mzazi wako.
  • Wasamaria wema kufika.
  • Ving’ora zaidi kupigwa.
  • Askari kufika.
  • Mapambano kati ya askari na wavamizi.
  • Kutoroka kwa baadhi ya wavamizi.
  • Kukamatwa kwa wengi wao.
  • Kupelekwa korokoroni.
  • Waliojeruhiwa kupelekwa hospitalini.
  • Tamati.