Ndege/Nyuni

 

Mifano ya Ndege/Nyuni

1. Heroe/ Flamingo - ndege wa jamii ya korongo anayepatikana sehemu zenye maziwa, mwenye miguu mirefu myekundu, shingo ndefu na mwili wa rangi nyeupe wenye wekundu.

2. Mbuni - ndege mkubwa mwenye miguu mirefu na shingo ndefu ambaye hawezi kuruka ila hukimbia kasi sana.

3. Kasuku - Ni ndege mwenye rangi nyingi anyeweza kuiga  maneno yanayosemwa na binadamu.

4. Chiriku - Ni aina ya ndege mdogo mwenye kelele nyingi.

5. Keremkeremu - Ni ndege mla asali.

6. Kereng’ende - Ni ndege mwitu ya jamii ya kuku lakini mmdogo mwenye rangi ya hudhurungi na miguu nyekungi.

7. Hudihudi - Ni aina ya ndege mdogo wa jamii ya njiwa mwenye mdomo mrefu na mwili wenye mistarimistari aliyemwambia Suleiman habari ya kuweko kwa Malaika wa Sheba.

8. Hondohondo - Ndege mkubwa kiasi mwenye rangi nyeusi na nyeupe na mdomo mkubwa mwekundu uliopinda.

9. Kanga - Ni ndege wa porini anayefanana na kuku mwenye mwili wa madoamadoa meupe na kichwa chenye upanga juu yake.

10. Njiwa/hua - Ndege ya jamii ya tetere au pungi lakini mkubwa anayekula nafaka mwenye rangi ya kijivu na nyeupe iliyopauka.

 

11. Kijimbimsitu (avuaye samaki baharini) - Ndege anayepata chakula chake kwa kupiga mbizi baharini na kukamata samaki.

12. Koleamiti 

13. Tai - Ndege mkubwa mwenye mdomo uliopinda nchani, kucha ndefu zilizokunjika na kali ambaye hula mizoga na wanyama wadogo kama panya.

14. Tetere - Ndege mdogo mithili ya njiwa na wa rangi ya kijivujivu mwenye alama kama ya pete shingoni.

15. Korongo - Aina ya ndege mwenye shingo na miguu mirefu anayependa kuishi sehemu zenye maji.

16. Mwewe - Ni aina ya ndege wa jamii ya tai ambaye hukamata vifaranga na kuku.

17. Bata - Ndege mkubwa kuliko kuku anayeishi porini au anayefugwa mwenye vidole vilivyounganishwa na vingozi vyembamba vinavyomwezesha kuogelea

18. Ngojamaliko - Ndege mkubwa mweusi mwenye tamvua jekundu shingoni anayependa kula nyoka na ambaye anafanana na korongo.

19. Bumu/bundi - Ndege mkubwa mwenye macho makubwa anayeruka usiku na hulaaniwa kuleta msiba.

20. Koho - Tai mla samaki.

21. Koikoi - Ndege mkubwa mwenye shingo ndefu, miguu mirefu na anyeishi karibu na maji.

22. Komakangi

23. Pwaju -  Ndege wa kahawia na kijani wa jamii ya mlembe mwenye kisuzu na mkia mwembamba.



  • bata by Nisqually delta restoration used under CC_BY-SA
  • Bumu-bundi by Pets lady used under CC_BY-SA
  • Chiriku by Digital journal used under CC_BY-SA
  • Flamingo by Anthrophysis used under CC_BY-SA
  • Hondohondo by WeShare used under CC_BY-SA
  • Kanga by pinterest used under CC_BY-SA
  • Kasuku by Design oval used under CC_BY-SA
  • Keremkeremu by Funmag.org used under CC_BY-SA
  • Kijimbimsitu by Birding buddies used under CC_BY-SA
  • Koho by HD Imagelib used under CC_BY-SA
  • Koikoi by Birds of North America used under CC_BY-SA
  • Mbuni by Safari Bookings used under CC_BY-SA
  • Mwewe by Live Science used under CC_BY-SA
  • Njiwa-hua by Beauty Birds used under CC_BY-SA
  • Pwaju by Birds of South Arabia used under CC_BY-SA
  • Tai by Wallpaper cave used under CC_BY-SA
  • Tetere by Bird Forum used under CC_BY-SA

  • Creative Commons License
    All work unless implicitly stated is licensed under a Creative Commons Attribution-NonCommercial-NoDerivatives 4.0 International License.