Ngeli ya U - ZI

- Ngeli hii inajumuisha nomino za vitu visivyo na uhai. Ngeli hii ina makundi matano ya nomino.

i. Nomino ambazo umoja huanza kwa u na wingi tunaondoa u k.m. unywele, ukuta, ufagio, ufunguo, unyasi, utepe, utosi, ukoo, upote, upenu, upondo, upongoo, upanga, upepeo n.k.

ii. Nomino ambazo umoja huanza kwa u wingi zinaanza kwa ny k.m. uta, ufa, uwanja, uso, uwayo, uzi, uwalio, ugwe.

iii. Nomino ambazo umoja huanza kwa w na wingi huanza kwa ny k.m. waraka, wakati, wembe, wimbo, wayo, waya, wavu, wanja, wanda, wadhifa, waadhi.

iv. Nomino ambazo umoja huanza kwa u na wingi huanza kwa nd k.m ulimi, uele.

v. Nomino ambazo umoja huanza kwa u na wingi huanza kwa mb k.m ubao – mbao, ubavu – mbavu, ubati – mbati, ubale-mbale

  • Vivumishi Kiwakilishi amba- Umoja: Ukuta ambao unakarabatiwa ni mrefu. Wingi: Kuta ambazo zinakarabatiwa ni ndefu.

  • “O” rejeshi

Umoja: Ukuta unaokarabatiwa ni mrefu.

Wingi: Kuta zinazokarabatiwa ni ndefu.

  • Ndi- ya kusisitiza

Umoja: Ufunguo huo ndio wangu.

Wingi: Funguo hizo ndizo zetu.

  • Si- ya kukataa

Umoja: Ufunguo huo sio wangu.

Wingi: Funguo hizo sizo zetu.

  • Na- ya kirejelei

Umoja: Utepe huu nao ni imara.

Wingi: Tepe hizi nazo ni imara.

 

  • Viashiria/vionyeshi

Umoja: huu huo ule.

Wingi: hizi hizo zile.

  • Viashiria/vionyeshi visisitizi

Umoja: uu huu uo huo ule ule.

Wingi: zizi hizi zizo hizo zile zile.

  • Viashiria/vionyeshi radidi.

Umoja: huu huu huo huo ule ule Wingi: hizi hizi hizo hizo zile zile.

  • Kivumishi -enye

Umoja: Uzi wenye fundo haushonei vizuri.

Wingi: Nyuzi z e n y e mafundo hazishonei vizuri.

  • Kivumishi -enyewe

Umoja: Ubao wenyewe unapendeza.

Wingi: Mbao zenyewe zinapendeza.

  • Kivumishi -ote

Umoja: Waya wote umetumika.

Wingi: Nyaya zote zimetumika.

  • Kivumishi -o-ote

Umoja: Nitautumia wavu wowote kuvulia.

Wingi: Tutazitumia nyavu zozote kuvulia.

  • Kivumishi -ngi

Umoja: Ameupokea waadhi mwingine.

Wingi: Wamezipokea nyaadhi nyingine

Wingi: Jirani amepokea nyaraka nyingi.

 

  • Kivumishi -ngine

  • Kiulizi -pi?

Umoja: Umesoma silabi za ukwapi upi?

Wingi: Mmesoma silabi za kwapi zipi?

  • Kiulizi –ngapi?

Wingi: Je, ng’ombe ana kwato ngapi?

  • Vivumishi vya idadi

Mmoja, mbili, tatu, nne, tano, sita, saba, nane, tisa, kumi, kumi na mmoja, kumi na mbili, kumi na tatu, kumi na nne, kumi na tano



  • a1_1 by en.wikipedia.org & eLimu used under CC_BY-SA
  • a2_2 by en.wikipedia.org & eLimu used under CC_BY-SA
  • a3 by bartleby.com & eLimu used under CC_BY-SA
  • a4 by flashbak.com & eLimu used under CC_BY-SA
  • a6 by mendocinobaby.com & eLimu used under CC_BY-SA
  • a10 by kesaus.org & eLimu used under CC_BY-SA
  • a8_1 by mustangsplus.com & eLimu used under CC_BY-SA
  • a9 by pinterest.com & eLimu used under CC_BY-SA

  • Creative Commons License
    All work unless implicitly stated is licensed under a Creative Commons Attribution-NonCommercial-NoDerivatives 4.0 International License.