Zana za vita

Hizi ni silaha zitumikazo wakati wa vita.

Mifano ya zana za vita.

1. Jeti: eropleni iendayo kwa kasi sana. Inatumika kupeleleza na hata kudondosha mabomu.

2. Bomu: silaha ambayo hulipuka na kuleta maafa makubwa.

3. Bunduki: silaha itumiwayo kufyatulia risasi.

4. Bastola: bunduki ndogo. Hushikwa na kufyatulia risasi kwa mkono mmoja.

5. Mzinga: silaha iliyo na mwanzi mkubwa ambao hutumiwa kurushia risasi. Ina nguvu kuliko bunduki.

6. Nyambizi/sabmarini: chombo cha kivita ambacho husafiri chini ya maji.

7. Manowari: meli ya kivita.

8. Kifaru: chombo mfano wa gari la chuma ambacho hutumika kwa vita.

9. Helikopta za kijeshi: eropleni iliyo na uwezo wa kutua popote. Huwa na panka juu.

10. Magari ya deraya: magari yawezayo kusafiri katika barabara mbovu na kwa kasi.

Mifano ya zana za vita.

11. Dereya/dirizi: nguo za vita zilizotengenezwa kwa chuma.

12. Parange: silaha mfano wa panga iliyo na makali upande uliopinda.

13. Korofindo: bunduki ya kushindilia gobori.

14. Panga: silaha mfano wa kisu.

15. Singe: kisu kinachochomekwa/kinachowekwa katika mtutu wa bunduki.

16. Sime: jisu lenye makali pande mbili.

17. Mkuki: silaha iliyochomekwa chuma ambacho kimechongoka.

18. Mshale: kijiti na chembe na hurushwa kwa upinde.

19. Kombeo/teo/kumbwewe: chombo cha kurushia mawe.

20. Guruneti

 

Aina za Silaha 



  • Bastola by Holliday used under CC_BY-SA
  • Bunduki by Tech Vision used under CC_BY-SA
  • Helikopta_za_kijeshi by wikimedia commons used under CC_BY-SA
  • Jeti by HNGN used under CC_BY-SA
  • Kifaru by Army Guide used under CC_BY-SA
  • Mzinga by Free stock photos.biz used under CC_BY-SA
  • Nyambizi-sabmarini by The National Interest used under CC_BY-SA
  • silaha by Swahili Land used under CC_BY-SA

  • Creative Commons License
    All work unless implicitly stated is licensed under a Creative Commons Attribution-NonCommercial-NoDerivatives 4.0 International License.