Malipo

- Malipo pia huitwa ada. Malipo hutolewa kutokana na shughuli mbalimbali. 

 

1. Karo: Ada ya shule inayotolewa na mwanafunzi.

2. Nauli: Malipo ya kusafiria.

3. Koto: Ada ya kumwingiza au kumsajili mwanafunzi shuleni.

4. Mahari: Malipo ya kuolea.

5. Fidia: Malipo kwa kusababishiwa hasara au maumivu.

 

6. Ridhaa: Malipo kwa ajili ya kuharibiwa sifa au jina.

7. Riba: Malipo kwa mkopo.

8. Pensheni: Malipo ya kustaafu (kiinuamgongo).

9. Arbuni: Malipo ya kwanza ya kununulia kitu/malipo ya kufungia kitu kisinunuliwe na mwengine.

10. Masurufu: Pesa za matumizi safarini au nyumbani.

 

11. Kiangazamacho: Zawadi kwa kuokota kitu kilichopotea.

12. Kodi ya mapato: Malipo kwa serikali kulingana na mapato ya mtu.

13. Ushuru wa forodha: Malipo kwa serikali kwa ajili ya kuuza au kuingiza bidhaa nchini.

14. Dia/arshi: Malipo kwa ajili ya kutolewa damu.

15. Kiingilio: Ada ya kuingilia michezoni.

 

16. Kivusho: Ada kwa ajili ya kutumia daraja au pantoni kuvukia.

17. Mapoza: Malipo kwa mtu aliyeudhiwa ili kutuliza hasira zake.

18. Kilemba: Malipo apewayo mhunzi na mwanafunzi wake baada ya kuhitimu mafunzo.

19. Tuzo: Zawadi apewayo mtu kwa kufanya jambo zuri.

20. Faini: Pesa za adhabu kwa kosa.


21. Dhamana: Fedha zitolewazo na mshtakiwa ili kuachiliwa kitambo kesi yake ikatwe.

22. Karisaji/ajari/ovataimu: Malipo ya pesa kwa muda wa ziada wa kufanya kazi.

23. Mrabaha: Malipo anayopewa mwandishi na kampuni iliyotoa kazi yake kila baada ya muda fulani wa mauzo.

24. Mchango: Malipo ya hiari ili kufanya shughuli fulani k.v. ujenzi wa shule.

25. Karadha: Mkopo usiotozwa riba.

 

26. Mshahara: Malipo ya mfanyikazi ya kila mwezi kwa kazi alioajiriwa.

27. Marupurupu: Malipo alipwayo mtu zaidi ya yale ya kawaida.

28. Ujira: Malipo kwa kazi iliyofanywa.

29. Fungule: Malipo kwa daktari.

30. Bahashishi: Zawadi kwa utumizi bora au huduma bora za kazi.

 

31. Kiokozi/kombozi: Malipo ya kukombolea kitu kilichotekwa nyara au kunyakuliwa.

32. Urithi: Mali yaachwayo na hayati na kupewa mtu fulani.

33. Rehani: Malipo ya kitu kilichowekwa dhamana ili kikombolewe baadaye.

34. Pango: Kodi ya nyumba au chumba anayolipa mpangaji kila mwezi au baada ya muda fulani.

35. Honoraria: malipo/ pesa kama bakshishi kwa kufanya kazi maalum. 

Eleza kiufupi malipo yafuatayo

a) Risimu       b) Fidia        c) Kibarua    d) Mtaji

e) Rushwa      f) Koto        g) Fichuo      h) kodi

i) Tapisho       j) Zaka        k) Mbiru    l) Mwago

m) Kudu       n) Mukafaa        o) Haka    p) Bakora

q) Kikunjajamvi       r) Kipkasa      s) Fola      t) Utotole     

u) Karisaji        v) Faida     w) Karadha (advansi)   

x) Rada            y) Thawabu