Heshima na adabu

Lugha ya heshima na adabu

- Lugha ya heshima hutumika kutajia mtu na hata mahali mbalimbali.

- Ni vizuri unapoongea na watu utumie maneno ya heshima la sivyo hata nawe hutaheshimiwa.

 

  • Siti: Jina la heshima la mwanamke. Hutumika kabla ya jina lake.
  • Bwana: Jina la heshima kwa mwanamume.
  • Bibi: Jina la heshima kwa mwanamke.
  • Nana: Jina la heshima ambalo hutumiwa kumwitia mwanamke.
  • Mwinyi: Jina la heshima ambalo hutumiwa kumwitia mwanamume.
  • Muadhama: Neno la heshima la kumwitia mtu maarufu (mheshimiwa)

  • Kibibi: Tamko la kumwita mtoto mwanamke.
  • Hayati: Marehemu:

Majina ya heshima ya kumtajia mtu

Mwendazake: aliyeaga dunia

Maneno ya heshima ya kuitikia

Abe hutumika na wanawake kuitikia wanapoitwa.

Bee, Beka, Naam: Neno la kuitikia kwa heshima.

Maneno ya adabu na unyenyekevu

  •  Tafadhali: Neno la heshima la kumwomba mtu afanye jambo kwa  niaba yako.
  •  Shikamoo: Salamu ya heshima itolewayo kwa mtu aliyekuzidi umri.
  •  Samahani: Neno la kuombea msamaha. Neno la kuomba upewe nafasi  au usikilizwe.
  •  Asante: Neno la kuonyesha shukrani kwa yale uliyotendewa.
  •  Ninasikitika:Neno la kuonyeshea hisia za huruma au kuionea hali ya  mtu huruma.
  •  Simile: Neno la adabu la kuomba kupishwa njia.
  •  Ashakum: Neno la kuombea msamha kabla ya kusema jambo  unalofikiria linaweza kumwudhi mtu anayekusikiliza.
  •  Mjamzito: Mwanamke aliyebeba mimba.
  •  Kujifungua:Kupata mtoto.
  •  Msalani/pembeni:Pahali pa kwendea haja.
  •  Pole: Neno la kumwonea mtu huruma au kumsikitikia kutokana na hali mbaya k.v. ugonjwa, kuumia n.k.