Vihisishi/ viingizi

- Vihisishi huonyeshea hisia za ndani. k.m.

• Hisia za mshangao.

• Hisia za huzuni.

• Hisia za furaha.

• Hisia za majuto.

• Hisia za huruma au masikitiko.

 

Tutumiapo vihisishi kihisi (!) hutumika. 

Mifano ya vihisishi

1. Lo! - hutumika kuonyesha mshangao, furaha, hofu au mshtuko na hali ya kubung'aa.

2. Masalale! -  huonyesha mshangao

3. Do! au Du! - huonyesha mshangao; hali ya kutoamini.

4. Salaala! - huonyesha mshangao wa hali ya juu.

5. Ebo! - huonyesha mshangao; hali ya dharau na kutoamini.

6. Aka! - huonyesha mshangoa; hali ya kukanusha jambo.

 

7. Ah! - huonyesha hali ya kukereka.

8. Ahaa! - huonyesha furaha; uchungu;kukubali;kukataa.

9. Aa! - huitikia; kukubali; kukataa; hali ya kuchanganyikiwa.

10. Po! - huonyesha dharau.

11. Pukachaka! - huonyesha kukidharau kitu; kutokithamini kabisa.

12. Oyee! - huonyesha furaha, shangwe na hali ya kupongeza.

 

13. Yarabi masikini! - hushangaa na kuomba msaadakwa mwenyezi Mungu.

14. Ewaa! - huonyesha kuitisha kuwa mambo ni sawa.

15. Hewaa! - hukubali kuwa mambo ni sawasawa;barabara!

16. Taib! - hukubali kuwa ni vyema au vizuri.

17. Shabash! - huonyesha furaha au mshangao wa hali ya kuridhishwa.

18. Ala! - huonyesha mshangao au mshtuko.

 

19. Aisee! - humfanya mtu asikilize unayotaka kumwambia; ohaa! abaa!

20. Cho! - huonyesha mshangao; lo! cha!

21. Chup! - humwambia mtu anyamaze kwa hasiraau dharau; kimya! chub!

22. Us! - humnyamazisha mtu kwa hasira au dharau.

23. Ehee! - huonyesha ukubaliano au hamu ya kuendelea kusikiliza; ehee!

24. Epuu! - huonyesha kutompa mtu hima ya kufanya au kutamka alilonuia; kutoamini analotamka.

 

25. Ewe! - huonyesha mshangao na mgutuko.

26. He! - huashiria wito wa kuhadharisha.

27. Aa-aa! - hunyamazisha, huzomea au kukemea.

28. Oh! - huonyesha mshangao; kutoamini yaliyosemwa.

29. Oofuu! - huonyesha uchovu au kuvuta pumzi kwa uchovu.

30. Mmh! - hali ya kutoamini unaloambiwa.

 

31. Afanalek! - huonyesha kupigwa na butwaa, kushtuka.

32. Audhubillahi! - huonyesha mshangao na kumlaani shetani.

33. Mnh! huashiria kuitikia kwa wasiwasi, hofu na mshangao.

34. Hee! - huonyesha mshtuko wa kutahadharisha au kuonya.

35. Ohoo! - hukashifu.

36. Zii! - hukemea; hulaani; kinyume cha kushangilia.

37. Yarabi Stara! - huashiria kuomba ulinza na Mwenyezi Mungu.

Zoezi

Tunga sentensi moja moja kuonyesha hisia za;

1. kukereka

2. kupongeza

3. kuhimiza

5. kunyamazisha

 



  • 9ik by Unknown used under Creative Commons Attribution-NonCommercial-NoDerivatives 4.0 International License
  • iuh by Unknown used under Creative Commons Attribution-NonCommercial-NoDerivatives 4.0 International License
  • ojoijoi by Unknown used under Creative Commons Attribution-NonCommercial-NoDerivatives 4.0 International License
  • ujn by Unknown used under Creative Commons Attribution-NonCommercial-NoDerivatives 4.0 International License

  • Creative Commons License
    All work unless implicitly stated is licensed under a Creative Commons Attribution-NonCommercial-NoDerivatives 4.0 International License.