Nafsi

Nafsi

Kwa lugha rahisi na ya moja kwa moja tunaweza kusema nafsi ni sawa na “mtu”. Katika lugha ya Kiswahili tunazo nafsi tatu:

  •  Nafsi ya kwanza. (mimi, sisi)
  •  Nafsi ya pili. (wewe, nyinyi)
  •  Nafsi ya tatu. (yeye, wao)

Nafsi ya kwanza Mimi – huwakilishwa na ni.

Sisi – huwakilishwa na tu.

Nafsi ya pili Wewe – huwakilishwa na u.

Nyinyi – huwakilishwa na m.

Nafsi ya tatu Yeye – huwakilishwa na a.

Wao – huwakilishwa na wa.

Viwakilishi

Kiwakilishi ni neno au silabi inayosimama badala ya nomino au kitenzi. Viwakilishi vya nafsi ni kama vifuatavyo.

Nafsi                                                            Kiwakilishi                                                 Matumizi

Nafsi ya kwanza

Mimi

Nitasoma kwa bidii

Sisi

Tutasoma kwa bidii

Nafsi ya pili

Wewe

Utasoma kwa bidii

Nyinyi

Mtasoma kwa bidii

Nafsi ya tatu

Yeye

Atasoma kwa bidii

Wao

Watasoma kwa bidii

 

 

 

Iwapo kitenzi kitanyambuliwa kiwe katika hali ya kufanyia, kiwakilishi cha wewe hubadilika kutoka u na kuwa ku. k.m

Utaandika barua (kufanya) - Nitakuandikia barua (kufanyia).

Yeye nacho huwa m badala ya a k.m. Alimcheka (kufanya) - Nilimcheka (kufanyia)

Viashiria vinaweza kutumika kama viwakilishi. Kiashiria huwa kiwakilishi kinapotumika badala ya nomino au kitenzi kinachoashiriwa. Kwa hivyo, hakitaandamana na nomino au kitenzi husika.

Ziangalie sentensi zifuatazo: Mtu huyu ana bidii - kiashiria Mtu huyu ana bidii, yule ni mzembe. Huyu – kiashiria Yule – kiwakilishi – kinawakilisha mtu wa pili (ambaye ni mzembe).