Majira

- Majira ni kipindi kirefu kiasi cha wakati.

- Aghalabu kipindi hiki huwa na hali fulani ya hewa.

- Masika/kifuku: Majira ya mvua tele ya mfululizo.

- Kiangazi/ukame: Majira ya jua kali.

- Vuli/mchoo: Majira ya mvua ndogondogo ambazo hupatikana wakati wa pepo za kaskazi.

- Kipupwe: majira ya baridi.

- Matlai: msimu wa pepo zinazovuma kutoka mashariki.