Maswali kadirifu

A. Jibu maswali yafuatayo kikamilifu.

Tumia haya maneno.

Bikari, panka, bilula, taipureta, jenereta, mtaimbo, milizamu, kitindio, panchi, kifyonzavumbi, uyoka, kamera, winchi, swichi, pantoni.

 

1. Chombo cha kutobolea mashimo karatasini ni ___________.

2. Chombo cha kutilia kisu makali ni ___________.

3. Chombo cha kuvunjia mawe na kuinulia vitu ni ___________.

4. Chombo cha kufungia au kufungulia maji mferejini ni ___________.

5. Mashine ya kuonyeshea vitu vilivyomo ndani k.v. chembe za mwili ni ___________.

6. Ufagio wa umeme utumiwao kwenye mazulia ni ___________.

7. Kifaa kidogo cha kunyofolea ndevu ni ___________.

8. Mashine madogo ya kutolea maandishi ni ___________. 

9. Chombo cha kupigia picha ni ___________.

10. Mtambo wa kutoa nguvu za umeme ni ___________.

11. Mtambo wa kuinulia mizigo mizito ___________.

12. Chombo cha majini cha kuvushia mizigo, watu n.k___________.

13. Kifaa cha chuma kizungukacho na kule•ta ubaridi ___________.

14. Kifaa kinachotumika kuzima au kuanzisha mkondo wa umeme kusambaa kwenye waya ___________.

15. Chombo cha kuchorea duara katika hesabu za maumbo ___________.

 

B. Eleza matumizi ya vyombo vifuatavyo.

1. Timazi

2. Msumari wa hesi

3. Pimamaji

4. Chenezo

5. Tumbuu

6. Pishi

7. Spana

8. Mtaimbo

9. Mizani

10. Mvukuto