Maswali kadirifu

Zoezi A

Linganisha kinyume cha jinsia ya neno katika (i) kutoka (ii) (i) 

Sehemu (i)

 

1. Baba           12. Fahali

2. Kaka           13. Mvuli

3. Mjomba      14. Njeku

4. Amu            15. Jogoo

5. Mgumba     16. Pora

6. Mtwana       17. Binamu

7. Bin                18. Babakambo

8. Shaibu          19. Mlamu

9. Kapera          20. Babu 1

10.Kungwi         21. Mwinyi

11.Ndenge       22. Mjane

 

Sehemu (ii)

a) Nyanya        l) Mori  

b) Kijakazi        m) Koo/mtetea

c) Banati           n) Ajuza

d) Nana             o) Mtamba

e) Nina               p) Mwanamwali

f) Binti               q) Dada

g) Mfarika         r) Halati

h) Nyakanga    s) Mfaruku

i) Wifi                t) Bintiamu

j) Tembe            u) Shangazi

k) Mamakambo  v) Tasa

 

Zoezi B

Jaza neno mwafaka ili kukamilisha jozi. 

Mfano: Mkemwenza ni kwa mwanyumba kama vile mjomba ni kwa shangazi

1. Mseja ni kwa ____ kama vile mtanashati ni kwa ______.

2. Tembe ni kwa _____ naye ______ ni kwa jimbi.

3. Mfalme ni kwa ________ naye Rais ni kwa _______.

4. Babu ni kwa ______ naye bamkwe ni kwa _______.

5. Kapera ni ______ kama vile ______ ni kwa kitwana.

6. Amu ni kwa _______ kama vile _______ ni kwa binti.

7. Fahali ni kwa ________ kama vile Litazame jedwali lifuatalo gumba ni kwa _______.

8. Bwana arusi ni kwa ______ kama jvile Mama Baba _____ ni kwa binti.

9. Ajuza ni kwa ______ kama vile wifi ni kwa _______.

10. Mume ni kwa _______ kama vile _______ ni kwa mama.

  

Zoezi C

Taja vinyume vya majina yafuatayo.

  • shaibu
  • hau
  • mwamu
  • sultan
  • maliki
  • kitwana
  • boi
  • kibwana
  • wadi
  • pakanunda
  • ami
  • mwanyumba
  • mtanashati
  • ghulamu
  • babu
  • jando
  • mwinyi
  • kapera
  • gumba
  • kirukamito
  • kijulanga
  • mwanaharamu
  • bikira
  • sahibu
  • nendaeka
  • kijana