Ngeli ya YA - YA

Ngeli ya YA-YA

Ngeli hii hujumuisha nomino za vitu visivyo na uhai.

Nomino za ngeli hii: • hubakia hivyo katika umoja na wingi, • hazihesabiki, na • huanza kwa silabi ma.

Mifano :

maji, mate, marashi, mafuta, madaraka, mamlaka, maisha, masuo, masira, maringo, maafa n.k.

Vivumishi

Vivumishi vya ngeli hii ni sawa na vile vya ngeli ya LI-YA (hali ya wingi) Muhimu Ngeli ya YA-YA, haina vivumishi visifa vya idadi wala kiulizi –ngapi?

 

Matumizi ya viambishi katika ngeli ya YA-YA

1. Viambishingeli ya - ya

i) Mazingira yangu yatunzwe. -  Mazingira yetu yatunzwe.

ii) Maisha yako yanapendeza. - Maisha yenu yanapendeza.

 

2. Kirejeshi-O- (yo-yo)

i) Maji yasiyotunzwa usiyanywe. - Maji yasiyotunzwa msiyanywe

ii) Mate ambayo yamo kinywani ni machungu. - Mate ambayo yamo vinywani ni machungu.

 

3. Kiunganifu -A (ya-ya)

i) Maliwato ya nyumba hii ni safi. - Maliwato ya nyumba hizi ni safi.

ii) Mafuta ya kumpaka mtoto yameisha. - Mafuta ya kuwapaka watoto yameisha.

 

4. Vivumishi -enye na enyewe (ye- ye)

i) Maskani yenye chakula chema. - Maskani Yenye vyakula vyema.

ii) Mazingira yenyewe ni yenye mti mzuri. - Mazingira yenyewe ni yenye miti mizuri.

 

5. Vizumishi -enye na -o-ote (yo -yo)

i) Majira yote ya masika yana mvua ya kutisha. - Majira yote ya masika yana mvua ya kutisha

ii) Madhara yoyote yanatisha. - Madhara yoyote yanatisha.

 

6. Sifa -eupe, -eusi n.k. (me -me)

i) Mafuta meusi si ya mtoto huyu. - Mafuta  meusi si ya watoto hawa.

ii) Maziwa si meusi ni meupe. - Maziwa si meusi ni meupe.

 

7. Sifa -ingi na -ingine (me-me)

i) Marashi mengi yanauzwa ghali dukani. - Marashi mengi yanauzwa ghali madukani.

ii) Mate mengine ni machungu kinywani. - Mate mengine ni machungu vinywani.

 

8) Vivumishi -zuri, -refu n.k (ma-ma)

i) Maziwa matamu ni mazuri kwangu. - Maziwa matamu ni mazuri kwetu.

ii) Maisha marefu ni bora kwa mtu kuliko mafupi. - Maisha marefu ni bora kwa watu kuliko mafupi.

 

9) Vikanushi (haya - haya)

i) Maji haya kunimwagikia. - Maji haya kutumwagikia.

ii) Majivuno hayana faida yoyote. - Majivuno hayana faida faida zozote.