Nomino ambata  by  Margaret Nguli

6

Nomino ambata huuundwa kwa nomino mbili (majina mawili) ambazo huambatanishwa na kuwa neno mja. Aghalabu maneno yanayounganishwa hayana uhusiano wowote kimaana.

Mifano

  • Askari + kanzu = askarikanzu
  • mwana + mkiwa = mwanamkiwa
  • Mwana +nchi = mwananchi
  • Mbwa + mwitu = mbwamwitu
  • Pembe + tatu = pembetatu
  • Kiinua + mgongo = kiinuamgongo
  • Nusu + kipenyo = nusukipenyo
  • Simba + marara = simbamarara

KUMBUKA ;maana ya neno yaweza kubadilika kabisa nomino mbili zinapoambanishwa.

MIFANO ZAIDI NA MAELEZO YAKE.

  • Simbamarara (a-wa) ____ fisi mkubwa.
  • Kivunjajungu (a-wa) ____ mdudu jamii ya panzi.
  • Mjamziti  (a-wa) ____ mwanamke aliyehimili.
  • Mtambaapanya(u -I) ____ mboriti (miti) inayoshikilia paa.
  • Kiamshakinywa (ki-vi) ____ chakula cha kwanza cha asubuhi.
  • Mwanambuzi (a-wa) ____ mtoto wa mbuzi.

ZOEZI

Tumia neno mwana kuunda nomIno ambata kumi.

Mfano
  • Mwana+ sheria = mwanasheria
  • mwana + mke = mwanamke

Tazama mifano zaidi

  • Mwana jeshi
  • Mwanasheria
  • Mwanaserere
  • Mwanamaji
  • Mwanandondi
  • Mwanadamu
  • Mwanambuzi
  • Mwanamkiwa
  • Mwanahewa