Maswahili kadirifu

Jibu maswali yafuatayo kikamilifu.

Tumia maneono haya. chemichemi, wangwa, tambarare, ziwa, nguu, kisiwa, upwa, migodi, kinamasi, msitu, gema, mto, nyika, jangwa, zilizala, delta

 

1. Mahali penye miti tele mikubwa kwa midogo, nyasi kwa vichaka ni _________.

2. Eneo kame ambalo halina nyasi wala miti ila mchanga ni _________.

3. Sehemu iliyo na nyasi na miti midogo ni _________.

4. Kilele cha mlima ni _________.

5. Eneo lenye maji mengi ambalo limezungukwa na nchi kavu ni _________.

6. Eneo la nchi kavu ambalo limezungukwa na maji huitwa _________.

7. Bonde lililo na maji yanayotiririka kila wakati hususan kuanzia mlimani kuelekea maeneo ya chini ni _________.

8. Mahali ambapo maji ya mto yanaanguka kwa kima kirefu toka juu ya mwamba ni _________.