Maumbile ya nchi
Maumbile ya nchi ni kama vile:
- Mto: Bonde lenye maji yanayotiririka wakati wote.

- Ziwa: Sehemu yenye maji mengi iliyozungukwa na nchi kavu.

- Bahari: Eneo kubwa la maji ya chumvi linalozungukwa na nchi kavu.

- Upwa: Sehemu ya pwani ambayo maji hujaa na hupwa.

- Delta: Sehemu mto unapojigawaganya vipande viwili au zaidi unapoingia baharini.

- Kinamasi: Mahali penye tope au telezi.

- Chemchemi: Mahali maji yanapobubujika.

- Gema/genge/korongo: mteremko mkali kwenye kingo za mto.

- Kisiwa: Eneo la nchi kavu lililozungukwa na maji.

- Msitu: Eneo kubwa lililo na miti mingi.

- Nyika: Sehemu inayoota nyasi na miti midogo.

- Jangwa: Eneo kubwa na kame ambalo kwa kawaida huwa na mchanga lisiloota nyasi wala miti.

- Tambarare: Nchi isiyokuwa na miinuko wala mabonde.

- Bonde: Sehemu ya ardhi iliyo katikati ya vilima viwili.

- Mlima: Sehemu ya ardhi iliyoinuka juu sana kuliko sehemu nyingine.

- Nguu: Sehemu ya juu kabisa ya mlima.

- Volkano: Mlipuko mkali wa moto unaotokea ndani ya dunia kumwaga zaha ambayo mara nyingi husababisha milima katika uso wa dunia.

- Kreta: Sehemu inayopatikana juu ya mlima. kifungulima:

- Kisima cha jangwani. Kisiwa: Eneo la nchi kavu lililozungukwa na maji.

- Wangwa: Sehemu ya pwani iliyo na mikoko ambapo maji hujaa na kupwa.

- Ghuba: Sehemu kubwa ya bahari iliyoingia ndani ya pwani.

- Mgodi: Mahali palipochimbuliwa madini.


- Kituka: Mahali penye miti mifupimifupi iliyoshonana na nyasi.
