Mahakamani

- Mahakamani ni mahali ambapo kesi na mashtaka mbalimbali huamuliwa. Pia huitwa kortini.

Msamiati wa hapa ni kama vile:

1. Hakimu/jaji – Huamua kesi au hutoa hukumu.

2. Mshtaki - aliyeleta malalamiko mahakamani

3. Mshtakiwa - anayedaiwa au kufikiriwa ndiye mwenye kosa.

4. Shahidi - anayetoa ushahidi. Aliyeona au kusikia tukio husika.

5. Wakili - Anayemtetea mshtaki au mshtakiwa.

6. Kiongozi wa korti (Mashtaka) – Anayemwongoza shahidi kutoa ushahidi. (Anayeongoza na kuelekeza mkondo wa kesi mahakamani)

7. Karani wa korti – Anayeandika matukio kortini (Anayeshughulikia barua na rekodi za kesi kortini)

8. Mshukiwa – anayedhaniwa kuwa amehusika katika uhalifu fulani.

9. Mahabusu – aliyehukumiwa kifungo gerezani/jelani.

10. Hakimu mkazi – hakimu anayeshughulikia mahakama fulani.

11. Mkuu wa sheria – mshauri mkuu wa serikali kuhusiana na mambo ya sheria.

 

12. Kiongozi wa mashtaka – wakili wa kuendesha na kuongoza mashtaka mahakamani.

13. Mdai – mlalamishi. Mtu anayepigania haki yake kutoka kwa mdaiwa.

14. Mdaiwa – mtu anayetakiwa alipe au arejeshe kitu cha mwingine.

15. Mtuhumiwa – mshukiwa anayefikiriwa amefanya kosa.

16. Kesi ya jinai – kesi iliyo na uzito mkubwa k.m. kesi ya mauaji.

17. Kesi ya uhaini – kesi kutokana na kupanga njama za kupindua serikali.

18. Ithibati – vitu vinavyowekwa au kutolewa mahakamani kama sehemu ya ushahidi.

19. Ahirisha kesi – kutangaza kesi isikilizwe siku au wakati mwingine.

20. Hatia – kosa linalostahili adhabu. (kosa mtu apatikanalo nalo).

21. Daawa – kesi dhidi ya mtu mmoja na mwengine.

 

22. Kuruka kesi – kukataa kukabiliana na mashtaka.

23. Kukata kesi – kutoa hukumu- kuamua kesi; kutangaza matokeo ya kesi.

24. Kata rufani – kuomba kesi isikilizwe upya.

25. Dhamana – malipo yanayotolewa na mshtakiwa ili aachiliwe huru kesi yake inapoendelea.

26. Faini – fedha inayotozwa kuwa ni adhabu kwa mwenye hatia.

27. Kizimba – sehemu katika korti anamokaa mshtakiwa, mshtaki au shahidi.

28. Hukumu – uamuzi katika kesi.

29. Korokoro – seli ya kufungia washukiwa katika kituo cha polisi.

30. Rumande – sehemu maalum katika jela wanapowekwa mahabusu ambao kesi zao hazijakamilika.

31. Jela – Sehemu ya kufungia mahabusu wanapotumikia kifungo chao.

32. Pingu/vikuku – vyuma aghalabu vya duara vya kufungia wahalifu hususan mikononi.