Kilimo

- Kilimo pia huitwa zaraa.

Yafuatayo yanahusiana na kilimo.

 

1. Shamba/konde – sehemu itumiwayo kukuzia mimea.

2. Kichaka – sehemu iliyo na miti na nyasi. Sehemu isiyolimwa.

3. Weu/ucheu – sehemu ya ardhi iliyolimwa kwa kupanda.

4. Kwekwe/magugu – nyasi na mimea iliyoota pasi kupandwa na huathiri mimea mingine ambayo imepandwa.

5. Makoongo – mashimo au mitaro ya kupandia mbegu au miche.

6. Miche – mimea michanga.

7. Kituta/kitangu – sehemu ya kukuzia miche kabla haijapandwa.

8. Kuo – Mstari wa miche

9. Kitalu – sehemu ya kukaushia mbegu.

10. Ghala – sehemu ya kuhifadhia mavuno hususan nafaka kavu k.v. mahindi.

 

11. Kufyeka – kukata na kuondoa nyasi na miti.

12. Kung’oa visiki – visiki ni sehemu ya chini za miti; sehemu ya shina na mizizi. Kwa hivyo   kung’oa visiki ni kuziondoa ardhini sehemu hizo.

13. Kulima muauta – kulima huku ukiinua matuta ya udongo juu.

14. Kulima sesa – kulima huku ukilainisha udongo.

15. Kupalilia – kulima huku uking’oa kwekwe na magugu.

16. Kutayarisha makoongo – kutayarisha mashimo au mitaro ya kupandia mbegu au miche.

17. Kupanda sia – kupanda mbegu bila kutayarisha makoongo/mashimo.

18. Kupandikiza/atika – kuung’oa mche na kuupanda sehemu nyingine.

19. Kupogoa – kuyakata na kuyapunguza matawi ya miti.

20. Kunyunyizia – kumwagilia maji kwa utaratibu.

21. Kuvuna/kuchuma – kutoa mazao ya mimea shambani.

Aina za mbolea

  •  Mbolea ya mitambo
  •  Mboji/matanda
  •  Samadi Kilimo cha mifugo kinahusu ufugaji. Baadhi ya mifugo ni kuku, mbuzi, ngamia, punda,bata, kondoo ng’ombe n.k.

Msamiati kuhusu mifugo

1. Maksai - ng’ombe dume aliyehasiriwa na hutumiwa kuburutia plau.

2. Mbuguma - ng’ombe anayeendelea kuzaa.

3. Njeku - ng’ombe dume ambaye bado hajawa fahali.

4. Ndenge - mbuzi dume mchanga.

5. Beberu - mbuzi dume.

6. Mori - ng’ombe jike ambaye bado hajazaa.

7. Mtamba/mfarika/dacha - mnyama wa kike ambaye amekomaa lakini hajazaa.

8. Jogoo/jimbi - kuku wa kiume aliyekomaa.

9. Koo/mtetea - kuku wa kike ambaye amekomaa.

10. Tembe - kifaranga wa kike.

 

11. Pora - kifaranga wa kiume.

12. Kiweto - koo asiye na uwezo wa kutaga mayai.

13. Kutaga - kutoa yai kutoka kwenye kiloakia.

14. Kuatamia - kalia au lalia mayai kama afanyavyo kuku ili yaanguliwe.

15. Angua/totoa - toa vifaranga ndani ya mayai.

16. Kunyonyoa - kuondoa nyoya za kuku.

17. Pepea - weka matunda palipo na joto ili yaive.

18. Yai viza - yai bovu lisiloweza kuanguliwa.

19. Kiangulio/kitotoa - mtambo wa kuangulia mayai ya kuku.

 

Vifaa vya kilimo

Kifaa 

Kazi

Fyekeo  Kufyekea nyasi
Jembe   Kuchimbia ardhi, kulimia.
Panga Kukatia miti, kuni.
Reki      Kuburura majani, kusawazisha udongo.
Haro    Kulimia.
Mundu    Kukatia miti.
Sepetu   Kuchotea mchanga.
Dodoki    Kusugulia mwili wakati wa kuoga.
Tingatinga  Kukokota vitu.
Glovu Kukingia mikono.
Shoka    Kupasulia kuni.
Plau    Kulimia.
Pigi    Kuangulia matunda.

 

Panga

Fyekeo

Jembe

Sepetu

Plau

Reki

Shoka