Ala za muziki

Ala za muziki ni vyombo vya kuchezea muziki.

 

Aina za ala za muziki

1. Ngoma: Ala ya muziki ambayo hutengenezwa kwa kuamba ngozi k.v. ya ng’ombe kwenye mzinga.

 

2. Tarumbeta: Ala ya muziki ya kupulizia ambayo vali zake hubonyezwa ili kubadilisha sauti.

 

3. Kinubi: Zeze ambalo lina nyuzi na hupigwa huku limesimamishwa.

 

4. Harimuni/kodiani: Kinanda ambacho hutoa sauti, kwa kubonyeza na kuvuta kwa mikono.

 

5. Manyanga: Chombo kilichowekwa vijiwe vidogovidogo kinachotumika kama ala ya muziki.

 

6. Njuga/msewe: Kengele ndogo zifungwazo shingoni, mkononi na hata miguuni wakati wa kucheza ngoma.

 

7. Saksafoni: Ala ya muziki ya kupuliza ambayo hubadilishwa sauti kwa kubonyeza vifungo vyake.

 

8. Mbiu: Pembe ya mnyama inayopulizwa wakati wa kucheza ngoma.

 

9. Gitaa/gita: Ala ya muziki ambayo hupigwa kwa vidole. Kwa kawaida, huwa na nyuzi sita.

10. Buruji: Tarumbeta ndogo.

11. Kayamba: Chombo chenye changarawe ndani na hutikiswa wakati wa kuimba.

12. Piano: Chombo cha muziki kilicho na vibanzi vinavyobonyezwa na kutoa sauti.

 

13. Fidla: Ala ya muziki mfano wa gita ndogo.

14. Filimbi: Chombo kitoacho sauti kinapopulizwa.

 

15. Marimba: Ala ya muziki mfano wa sanduku hutengenezwa kwa mbao na vibao vyembemba hutandikwa. Vipigwapo kwa virungu viwili hutoa sauti.

 

16. Zeze: Ala ambayo ina nyuzi kama za gita.

17. Tari/dafu: Ngoma ndogo iliyoambwa upande mmoja na kuwekwa vibati kwenye kingo zake.

18. Nai: Ni ala iliyo na umbo la filimbi ingawa haina tundu nyingi.

 

19. Baragumu: Pembe kubwa iliyotobolewa shimo ndogo karibu na ncha yake.

20. Zumari/Nzumari: Ala ya muzik iambayo ni nyembamba mdomoni na pana upande unakotokea sauti. Tundu hutoa sauti mbalimbali.

21. Upatu: Chombo chenye umbo la sinia, cha chuma kipigwacho na kutoa sauti.

22. Gambusi: Ala ya muziki ifananayo na banjo.

23. Msondo: Ngoma ndefu na kubwa.

24. Chapuo: Ngoma ndogo iliyowambwa pande zote mbili.

25. Udi: Ala ya muziki inayofanana na gita bali ni pana upande.

26. Banjo: Ala ya muziki iliyo na nyaya nne au zaidi. Ina shingo ndefu na kitako kipana.

27. Kuro: Ngoma kubwa inayosimama kwa miguu mitatu.



  • Gitaa by ebay used under CC_BY-SA
  • Kinubi by Salvi harps used under CC_BY-SA
  • Kodiani by pinterest used under CC_BY-SA
  • Manyanga by Free coloring pages used under CC_BY-SA
  • Mbiu by wikipedia used under CC_BY-SA
  • Ngoma by African museum used under CC_BY-SA
  • saksofoni by Sam Newsome's used under CC_BY-SA
  • Tarumbeta by Life Daily used under CC_BY-SA
  • african-kayamba by Motherland curious used under CC_BY-SA
  • Filimbi by Seron used under CC_BY-SA
  • Marimba by Grocotts used under CC_BY-SA
  • Piano by Stanford used under CC_BY-SA
  • Zumari by Parade used under CC_BY-SA
  • K.4.24.3 by Unknown used under Creative Commons Attribution-NonCommercial-NoDerivatives 4.0 International License

  • Creative Commons License
    All work unless implicitly stated is licensed under a Creative Commons Attribution-NonCommercial-NoDerivatives 4.0 International License.