Maswali kadirifu

Jaza mapengo yafuatayo

 

1. Mtu aliye na dosari kwenye viungo vya mwili huitwa _____.

2. Mtu aliyepofuka jicho huitwa _____.

3. Mtu aliyepofuka macho yote mawili huitwa ______.

4. Mtu asiye na meno yote kinywani huitwa ______.

5. Mtu aliye na meno machache kinywani huitwa _____.

6. Mtu aliyezaliwa na meno huitwa _____ au ______.

7. Mtu anayezungumza na ncha ya ulimi huitwa _____ au _____. 

8. Mtu aliye katika kidole huitwa _____.

9. Mtu aliyevia huitwa _____.

10. Mwanamke asiyeweza kuzaa huitwa _____.

 

11. Mwanaume asiyesimika au ambaye jogoo lake haliwiki huitwa _____.

12. Mtu asiye kuwa na rangi kamili ya ngozi huitwa _____.

13. Mtu hasa mtoto anayetabawali kwenye malazi huitwa _____.

14. Mtu aliye na meno yaliyopandana kinywani huitwa _____.

15. Mtu aliyepindika miguu kama uta huitwa _____.

16. Mtu asiyeweza kuongea huitwaje _______.

17. Mtu asiyeweza kusikia huitwa ________ au ________.

18. Mtu aliyekatika nyama za pua huitwa _______.

19. Mtu aliyekatika nyama za ndewe huitwa _________.

20. Mtu anayeongea/zungumza kwa kusitasita au kudodosa maneno huitwa ______ au _______.

 

21. Mtu asiye na nywele kichwani huitwa _______.

22. Mtu ambaye nywele zake hung'oka ovyoovyo huitwa _______ au _______.

23. Mtu aliye na nundu mgongoni huitwa ______, ______, ______, ______, _______ au _______.

24. Mtu aliyepindika vidole vya miguu au mikono huitwa _______.

25. Mtu aliyekatika mkono huitwa ________.

26. Mtu aliyekatika vidole huitwa ________.

27. Mtu aliye na mguu mmoja huitwa _______.

28. Mtu aliyelemaa miguu yote miwili na anatembea kwa kusota au kukweta huitwa ________.

29. Mtu mfupi kimaumbile huitwa _______, ______, ______, ______ au ______.

30. Mtu ambaye miguu yake imepindika nje huitwa ________.

 

31. Mtu ambaye amepindika miguu yake kwa ndani huitwa _______.

32. Mtu aliye na miguu iliyopindika kama uta huitwa ______.

33. Mtu aliye na meno yaliyopandana kinywani huitwa ________.

34. Mtu anayezungumza kwenye pua huitwa kipua au ________. 

35. Mtu mwenye viungo vyote vya uzazi cha kiume na kike huitwa ________.

36. Mtu hasa mtoto anayetabawali kwenye malazi huitwa _________. 

37. Mwanamume asiyekuwa na mbegu za uzazi huitwa _________.

38. Mwanamke asiyeweza kuzaa huitwa __________.

39. Mtu asiyekuwa na rangi kamili ya ngozi huitwa _________.

40. Mwanamume asiyesimika au ambaye jogoo lake haliwiki huitwa ___________.