Viashiria na viulizi pamoja na ngeli  by   

Viashiria ni nini?

Viashiria ni kivumishi kinachotumiwa kuonyesha kwa kutegemea mahali kulipo kitu kinachoonyeshwa aidha huitwa kionyeshi.

Aina ya viashiria

  • Kiashiria cha karibu - HAPA
  • Kiashiria cha mbali kidogo - HAPO
  • Kiashiria cha mbali sana - PALE

MIFANO KATIKA SENTENSI

  • Mbuzi huyu ni mnono kuliko yule.
  • Mbuzi hawa ni wanono kuliko wale.
  • Kiu chako hicho si kama chake.
  • Embe lile linafanana na hilo.
  • Maembe yale yanafanana na hayo.

ZOEZI

  • Giza ____ (hilo,hiyo,hicho,huo) lilitutisha,
  • Nitakupa vifaa ____ (zako, vyako,yako, chako) sasa hivi.
  • uji ____ (yake, wake, lake, zake) umemwagika.
  • Amechukua kuni ____ (yake, zake, chake, kwake) akaenda
  • Nyumbani ____ (zile, yale,pale,ile) hupendeza.
  • kusafiri ____ (yake, wake, zake, kwake) kulimfurahisha.

MAJIBU

  • HILO
  • VYAKO
  • WAKE
  • ZAKE
  • PALE,
  • KWAKE