Biashara

- Biashara inahusu ununuzi na uuzaji wa bidhaa na/au huduma.

- Mifano ya bidhaa ni kama vile nguo, magari, chakula n.k.

- Mifano ya huduma ni kama vile bima, simu n.k.

- Kwa kawaida lengo la msingi la kufanya/kupiga biashara ni kupata faida ingawa mara kwa mara, hasara hupatikana.

- Biashara inaweza kuwa ya kitaifa (hufanywa katika taifa moja) na pia ya kimataifa (hufanywa baina ya mataifa zaidi ya moja).

 

Msamiati wa biashara

1. Faida/tijara/kivuno/chumo/ziada - Pato libakialo baada ya kuondoa gharama za kufanya biashara k.v. ununuzi na usafirishaji.

2. Hasara -Ukosefu wa faida; Hali ya kupoteza pato au mali katika biashara.

3. Bei -Kiwango cha pesa kununulia au kuuzia bidhaa au huduma fulani.

4. Uuzaji wa rejareja -Uuzaji wa kiasi kidogo kidogo.

5. Uuzaji wa jumla - Uuzaji wa kwa pamoja.

6. a) Bei rafi - Bei ambayo haipunguzwi.

b) Kipimo rafi - Kipimo ambacho hakipunguzwi.

c) Bei ya kuruka - Bei isiyokubalika kisheria/haramu.

7. Raslimali - Ujumla wa mali yaanyomilikiwa na mtu au nchi.

8. Malighafi -Mali yanayotumika kutengeneza vitu vingine k.m. pamba ni malighafi ya kutengenezea nguo.

9. Maliasili -Utajiri kama vile madini, misitu, maziwa, mito, anga vinavyopatikana katika mazingira.

10. Uwekezaji - Kutumia pesa/mali ili kuzalisha fedha/mali zaidi.(ilikupata faida).

 

11. Kitegauchumi - Rasilmali k.v. kiwanda inayotumika kuzalisha mali.

12. Ujasiriamali -Uwekezaji mtaji katika biashara.

13. Mtaji -Mali ya kuanzisha biashara au kuipanulia.

14. Ulanguzi -Ufichaji wa bidhaa ili bei yazo iruke.

15. Magendo -Upigaji biashara kwa njia haramu/isiyo halali.

16. Chenji -Pesa zinazobaki baada ya kununua kitu.

17. Maduhuli - Bidhaa ambazo hununuliwa kutoka nchi za nje.

18. Mahuruji - Bidhaa zinazouzwa nchi za nje.

19. Ushuru - Kodi ya kuingiza bidhaa nchini au kuziuza/Ada ya forodha.

20. Ruzuku - Pesa zinazotolewa na serikali kwa idara mbalimbali ili kujiendeleza.

 

21. Mshtiri - Mnunuzi.

22. Mteja - Aendaye kununua bidhaa au huduma.

23. Wakala - Ajenti.

24. Utandawazi -Utaratibu wa mataifa kushirikiana katika nyanja mbalimbali k.v. biashara.

25. Ubinafsishaji -Hali ya kusababisha mali ya umma imilikiwe na watu binafsi.

26. Ubia -Ushirikiano wa watu wawili au zaidi katika shughuli k.v. ya biashara.

27. Hawala - Hundi/cheki.

28. Amana - Kitu unachomwekea mwenzako hadi atakapokihitaji.

29. Turuhani/kipunguzo – Kiwango kinachotolewa kutoka katika bei iliyotangazwa.

30. Ikfisadi -Uangalifu katika kutumia fedha/mali.

 

31. Ubepari -Mfumo wa uchumi ambao unawawezesha watu wachache kumiliki raslimali na vitegauchumi.

32. Ukiritimba -Hali ya kuzuia wengine kufanya biashara au kushindana katika biashara.

33. Dukakuu - Duka kubwa ambapo wateja hujichukulia bidhaa watakazo kutoka rafuni.

34. Hisa - Sehemu ya mtaji katika biashara.