Maswali kadirifu

A. Andika jibu mwafaka.

1. Chumba cha kufanyia utafiti wa kisayansi ni ____________.

2. Chumba cha wanafunzi cha kulia huitwa ______________.

3. Mahali pa kuokea vyungu huitwa ____________.

4. Sehemu ya kuhifadhi nafaka ni __________.

5. Nyumba ya kujilindia kutokana na adui huitwa _________.

6. Ukumbi wa mazungumzo huitwa _________.

7. Mahali k.v meza pa kutolea huduma mbalimbali huitwa _________.

8. Mahali pa kushuka pwani kutoka melini huitwa ____________.

9. Mahali panapouzwa chai: kahawa na vyakula vingine huitwa ______.

10. Mahali pa kutengenezea vyombo vya usafiri huitwa _________.

 

11. Chumba cha kupigia na kurushia picha huitwaje? __________.

12. Wanyama hupelekwa __________ kula.

13. Mahali ambapo wanyama huchinjiwa huitwa _______________.

14. Sehemu ambapo mtu huenda haja ni ________________.

15. Mahali ambapo wavulana hutahiriwa huitwaje? ___________

16. Mahali panapouzwa chakula na vinywaji k.v katika shule huitwa ____________.

17. Duka la vipodozi na utengenezaji wa nywele huitwa _______________.

18. Mahali pa kuogeshea mifugo k.v. mbuzi na ng’ombe huitwaje? ______________.

19. Nyumba ya kulala wanafunzi katika shule au chuo huitwa _____________.

20. Mahali pa kupikia ni _______________.