Maswali kadirifu

A. Tumia nomino za makundi sahihi kati ya haya kujaza mapengo

Vipeto, hombo, madonge, matopa, majora, minofu, jumuia, mashunge, matuta, tita. 

 

1. Mama alinunua ______ la samani.

2. Wasasi waligawana ____ ya nyama.

3. Msomi huyo alikuwa na _____ ya vitabu.

4. Tarishi alibeba _____ vya barua.

5. Shambani kulionekana ____ ya udongo.

6. Nilimwona mjakazi aliyebeba ____ la kuni.

7. Washonaji walinunua ____ ya vitambaa.

8. Jitu hilo lilibugia ____ ya sima.

9. Tuliyakata ____ ya mpunga.

10. Viongozi wa _____ ya madola walikutana jijini.

 

B. Tumia majibu mwafaka kujaza mapengo.

1. Mnamo msimu wa kiangazi mawingu ya __________ yalionekana angani.

2. Tuliliona ______ la ng’ombe huko malishoni.

3. Wakati wa usiku ______ za nyota zilionekana mbinguni.

4. Mrembo huyo alikuwa na ______ ya vipuli ndeweni.

5. ______ la mawaziri lilikutania huko ikulu.

6. Wezi hao walitiwa mbaroni wakiwa na ______ vya nguo vya wenyewe.

7. Mchuuzi huyo alibeba ________ ya mayai.

8. Seremala yule alinitengenezea _______ ya fanicha ya kifahari.

9. _______ hilo la takataka lilinuka fee!

10. Akina mama hao walitunukiwa ____ ya leso.

 

11. Kijana huyo alijuta aliporushia _______ wa nyuki mawe.

12. Wachapishaji walikuwa na ________ ya karatasi.

13. Barabarani kulionekana ________ wa magari.

14. __________ cha wachawi kulifumaniwa huko mwituni kikipanga njama.

15. ________ la waandishi lilikutana kurati•bu mikakati ya uandishi.

16. Mwanamke huyo alikuwa na _________ la nywele la kupendeza.

17. Tuliyameza __________ ya maji ili kukatia kiu.

18. _________ cha askari kilifika kuzima ghasia za wagomaji.

19. Muthoni ameteuliwa kwa ____ ya shule.

20. Shangazi Nyokabi atanunua ________ ya sahani.